KIRAI NOMINO KATIKA KIPEMBA: UCHANGANUZI WA KIMUUNDO

No Thumbnail Available

Date

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

SUZA

Abstract

Description

Utafiti huu umechunguza virai nomino katika Kipemba. Uchanganuzi wa kimiundo na umegawanywa katika sura tano. Sura ya kwanza ni utangulizi ambao unajumuisha vipengele vya awali vya utafiti.Vipengele vilivyoelezwa katika sura ya kwanza ni usuli wa tatizo, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti na mipaka ya utafiti.Sura ya pili imeeleza mapitio ya machapisho na kiunzi cha nadharia, ambapo imetumika nadhari ya Sarufi jumuishi miundo virai (19). Aidha, sura ya tatu imejadili mbinu na njia za utafiti, vifaa vya utafiti, ukusanyaji wa data na uwasilishaji wa data. Mbinu zilizotumika katika utafiti huu ni usaili, uchunguzi makini na hojaji. Sura ya nne imehusiana wa uchambuzi wa data ambao ulihusisha malengo matatu, ambapo lengo la kwanza ni ubainishaji wa miundo ya virai nomino katika Kipemba. Lengo la pili ni kufafanua utokeaji wa miundo ya virai nomino katika Kipemba. Na lengo la tatu ni kuchambua miundo ya virai nomino katika Kipemba kwa mujibu wa nadharia iliyotumika katika utafiti huu ambayo ni Sarufi jumuishi muundo virai. Sura ya tano inaelezea matokeo ya utafiti huu, ambapo Kipemba kinaonesha kuwa kina miundo ya virai nomino ambayo inaonesha muunganiko wa nomino na viwakilishi au nomino na vivumishi ambapo husimama pamoja na kuunda tungo kirai. Vivumishi hivyo huweza kushikana na nomino au viwakilishi na huanzia na kimoja, viwili hadi vitatu
Utafiti huu umechunguza virai nomino katika Kipemba. Uchanganuzi wa kimiundo na umegawanywa katika sura tano. Sura ya kwanza ni utangulizi ambao unajumuisha vipengele vya awali vya utafiti.Vipengele vilivyoelezwa katika sura ya kwanza ni usuli wa tatizo, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti na mipaka ya utafiti.Sura ya pili imeeleza mapitio ya machapisho na kiunzi cha nadharia, ambapo imetumika nadhari ya Sarufi jumuishi miundo virai (19). Aidha, sura ya tatu imejadili mbinu na njia za utafiti, vifaa vya utafiti, ukusanyaji wa data na uwasilishaji wa data. Mbinu zilizotumika katika utafiti huu ni usaili, uchunguzi makini na hojaji. Sura ya nne imehusiana wa uchambuzi wa data ambao ulihusisha malengo matatu, ambapo lengo la kwanza ni ubainishaji wa miundo ya virai nomino katika Kipemba. Lengo la pili ni kufafanua utokeaji wa miundo ya virai nomino katika Kipemba. Na lengo la tatu ni kuchambua miundo ya virai nomino katika Kipemba kwa mujibu wa nadharia iliyotumika katika utafiti huu ambayo ni Sarufi jumuishi muundo virai. Sura ya tano inaelezea matokeo ya utafiti huu, ambapo Kipemba kinaonesha kuwa kina miundo ya virai nomino ambayo inaonesha muunganiko wa nomino na viwakilishi au nomino na vivumishi ambapo husimama pamoja na kuunda tungo kirai. Vivumishi hivyo huweza kushikana na nomino au viwakilishi na huanzia na kimoja, viwili hadi vitatu
SUZA

Keywords

KIRAI NOMINO KATIKA KIPEMBA: UCHANGANUZI WA KIMUUNDO

Citation